WAY

Monday, November 3, 2014

SERIKALI KUKAMILISHA UJENZI WA HOSPITAL YA RUFAA MKOANI MARA

          Ujenzi wa Hospital ya Rufaa Mkoani Mara
Tatizo kubwa la ukosefu wa huduma za afya za rufaa ambalo limekuwa likichangia vifo vingi kwa wananchi wa mkoa wa mara nchini Tanzania ,limeanza kupatiwa ufumbuzi baada ya serikali kuanza ujenzi wa hospitali kubwa ya rufaa ya Mwalimu Nyerere Medical Center katika eneo la Kwangwa manispaa ya Musoma mkoani humo.

Akipokea madaktari bingwa wa magonjwa mbalimbali yakiwemo ya moyo,upasuaji na wanawake na watoto ambao wamepelekwa mkoani Mara kupitia mpango wa mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya ili kusogeza huduma za madakari bingwa kwa wananchi wa mikoa wa pembezoni, Mgaga mkuu wa Hospatal ya Mkoa wa Mara Samson Winani amesema tayari Serikali imenza utekelezaji wa ujenzi wa hospitali hiyo.
kwa upande wake mwakilishi wa Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya Bw Michael Kishiwa,amesema mfuko huo umechukua uamuzi wa kupeleka madakatari bingwa katika mikoa ya pembezoni baada ya kubaini idadi kubwa ya wananchi wamekuwa wakipoteza maisha kwa kukosa uwezo wa kifedha kwa ajili ya kutafuta huduma za matibabu za rufaa.
--

0 comments:

Post a Comment

.

.

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...