WELCOME TO GMBONGO BLOG

To keep the body in good health is a duty... otherwise we shall not be able to keep our mind strong and clear.

TANGAZA NASI SASA

Tuwasiliane kwa Email: gmbongo.chuma@gmail.com

WE ARE HERE TO SERVE YOU

Keep you Entertained always

WE ARE HERE TO SERVE YOU

Habari na Burudani

WELCOME TO GMBONGO WORLD

Kwa habari za Burudani na zenye uhakika.

WAY

Sunday, January 25, 2015

MWIGIZAJI WA FILAMU ZA KISWAHILI ASHELY TOTO AZUA UTATA WA AMBER ROSE MITANDAONI PICHA ZAKE ZASAMBAA

jmmaa
Mwigizaji tena promoter wa muziki raia wa Kenya ambaye makao yake yako nchini Ujerumani, Ashley Toto, amewaacha midume vinywa wazi baada ya picha zake za kitandani kuvuja kwenye mitandao ya kijamii huku sehemu muhimu za mwili wake zikiwa wazi.
10893289_10205138225722838_1824582473_o
Ashley Toto anayetamba katika filamu ya Moyo wangu aliyo higiza pamoja na wasanii wa V.A.D Production nchini Danmark, alikuwa matembezini katika nchi ya Mweshimiwa Jakaya Kikwete kwa mipangilio ya mahandalizi ya kucheza filamu pamoja na waigizaji wa nchi hiyo ya Tanzania.

Thursday, January 22, 2015

JESHI LA POLISI LAZINDUA MPANGO WA KUKABILIA NA MAJAMBAZI GEITA,KAGERA NA KIGOMA

    Kamanda wa polisi mkoa we Kagera Kamishna msaidizi mwandamizi wa polisi Henry Mwaibambe  
JESHI la Polisi mikoa ya Kigoma,Kagera na Geita limezindua mpango endelevu wa kuuangamiza mtandao wa uhalifu wa kutumia silaha kwa kuwatahadharisha wananchi kuepukana na tabia ya kuwakarimu wageni wanaowatilia mashaka na badala yake wawaripoti Polisi au kwa mamlaka zingine.

Tahadhari hiyo imetokana na baada ya wananchi wa Kitongoji cha Mhama, kijiji cha Ilyamchele Wilayani Bukombe Mkoani Geita Januari 19 mchana kujikuta wakiwakirimu majambazi wakiwemo kutoka nchi jirani kwa chakula na vinywaji wakidhania ni Askari wa hifadhi kutokana na nguo walizokuwa wamevaa kufanana na sare za Askari wa hifadhi kumbe ni majambazi kabla ya kuwageuka na kutoa silaha za kivita na kuwapora.

Sanjari na kuchukua tahadhari hiyo wananchi wameombwa kutoa ushirikiano kwa polisi kwa kutoa taarifa za siri zitakazoiwezesha polisi kuwanasa watu wote wanaoendesha vitendo vya uhalifu wakiwemo wanaowaficha na wanaoshirikiana na watu kutoka nchi jirani katika mikoa ya Kagera,Kigoma na Geita.
        Kamanda wa Polisi mkoa wa Geita Kamishna msaidizi mwandamizi wa polisi Joseph Konyo
Kamanda wa Polisi mkoa wa Geita Kamishna msaidizi mwandamizi wa polisi Joseph Konyo amesema hayo leo baada ya kikao maalum kati ya Kamanda wa polisi mkoa we Kagera Kamishna msaidizi mwandamizi wa polisi Henry Mwaibambe cha kuzindua mkakati kabambe wa kuusaka mtandao wa uhalifu kilichonfayika katika kijiji cha Nyakanazi Wilayani Biharamulo Mkoani Kagera Juzi januari 20.
‘’Wananchi wabadilike ..kama siyo mjambazi hao kuingiwa na hofu baada ya kupata taarifa ya kuwepo porini kwa Kikosi cha kupambana na Uhalifu wa kutumia Silaha cha mkoani Geita majambazi hao wangeweza kufanya kufuru lakini kwa kuhofia hilo waliamua kufyatua risasi juu na kisha kuiba mchele kilo 60 na baiskeli tatu walizotumia kubebea mchele walioiba kabla ya kuzitupa kwa kuhofia kukutana na kikosi cha Antroberry’’alidai Konyo.

Aliongeza majambazi hao wanadaiwa walifika katika kijiji hicho wamevaa nguo zinazofanana na sare za Askari wa hifadhi na wanakijiji waliwakarimu kama watumishi wa serkali kwa kuwanunulia chakula na vinywaji lakini mwanakijiji mmoja aliwadokeza wenzake kuwa wale watu pamoja na kuvaa sare za Askari wa hifadahi kwa juu lakini ndani walikuwa wamevaa sare za jeshi kama la wananchi Jwtz lakini wenzake walimpuuza.

‘’Baada ya kukirimiwa pombe na chakula ghafla watu hao walitoa bunduki za kivita ikiwemo bunduki nzito inayodaiwa kuwa Light Mchine Gun[LMG]na kuwaamuru wananakijiji waliokuwepo kukaa chini ya ulinzi kwa muda kwa kufyatua risasi hewani na kisha kuondoka na kilo 60 za mchele na baiskeli tatu ambazo baadaye walizitupa wakihofia kunaswa’’alisema Konya
Wakati wakitoka eneo la tukio wakiondoka majambazi hao walichoma kibanda[Kijumba]kwa moto kwa lengo la kuwafanya wanakijiji wasiwafuate na badala yake washughulikie uzimaji moto kibanda kile na ndicho kilichofanyika na wakatumia fursa hiyo kutoweka huku wanakijiji wakiwarushia mishale bila ya mafanikio.
Kamanda Konyo alisema uchunguzi wa kiintelijensia umebaini watu hao walivuka na kuingia nchi jirani bila ya kuitaja kwa sababu za kiupelelezi…na ni sehemu ya mtandao ambao umekuwa unaedesha uhalifu katika mikoa ya Kagera,Kigoma na Geita huku pori la akiba la Kigosi lililopo wilayani Bukombe linalopakana na wilaya za Biharamulo mkoani Kagera na mkoa wa Kigoma likitumiwa kama maficho ya wahalifu hao.
Hata hivyo watu hao walitupa baiskeli hizo baada ya kuhofia kukutana na Askari wa kikosi maalum cha kupambana na Uhalifu wa kutumia silaha[Ant-robberry]na kufanikiwa kutokomea kabla ya Askari kufika eneo la tukio hata hivyo taarifa zilizokwishapatikana za kiintelijensia zimedaiwa zitasaidia kuunasa mtandao huo na kuwataka wahalifu wote kujisalimisha wao au silaha zao kwani siku zao zimehesabiwa kutoka sasa iwapo wananchi nao watasimama kidete kutoa ushirikiano kuwafichua wahalifu hao kwani wanawatambua na baadhi wanaishi nao.
Inasadikiwa mtandao huo ni sehemu ya mitandao ya uhalifu wa kutumia silaha iliyopo katika Miji ya Lunzewe,Namonge,Kasanda na Mabamba iliyopo katika mikoa ya Geita,Kagera na Kigoma na baada ya hapo huvuka na kuingia nchi jirani na hushirikiana na wenyeji ambao wao huratibu utekelezaji wa matukio hayo na wageni huja kutekeleza.
Kikosi nguvu kazi hicho kitakachowashirkisha makachero na wale wa Kikosi cha kupambana na unyang’anyi wakutumia silaha katika mikoa mitatu kitakuwa kiungo mhimu katika utekelezaji mkakati huo huku ukiwemo mfumo wa kubadilishana taarifa za uhalifu na zile za kikachero’’kiintelejensia’’katika mikoa hiyo mitatu kwa lengo la kuufyeka kabisa mtandao huo ambao umekuwa kero kubwa katika mikoa ya Geita,Kagera na Kigoma
Hata hivyo wadau waliohojiwa mkoani Geita kwa masharti ya kutotajwa majina yao juu ya hali ya uhalifu mkoani humo wamesema idadi ya matukio ya uhalifu wa kutumia silaha yamepungua ikilinganishwa na miaka miwili iliyopita kulikochangiwa na ushirikishwaji wa wananchi kwa kuhakikishiwa usalama wao katika kufichua uhalifu…baada ya kutoa taarifa za siri badala ya kusalitiwa na Askari wasio waadilifu kwa kuzigeuza kuwa dili.

Wamesema hatua hiyo inatokana na Timu madhubuti iliyopikwa na uongozi uliopo sasa wa polisi mkoani hapa kwa kurejesha imani kwa wananchikwa kuwalindawatoa taarifa za siri na kusikilizwa,pia kikosi cha Kuapambanana uhalifu wakutumia silaha kimekuwa imara wakati wote tofuati na awali.

Mwaka jana watu wanaosadikiwa kuwa majambazi walivamia kituo kikuu cha polisi wilaya ya Bukombe Mkoani Geita na kuua Askari wawili na kupora silaha,lakini kutokana na ushirikiano kati ya polisi na wanachi watuhumiwa waliweza kukamatwa pamoja na silaha zote zilizokuwa zimeibiwa.

.

.

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...