WELCOME TO GMBONGO BLOG

To keep the body in good health is a duty... otherwise we shall not be able to keep our mind strong and clear.

TANGAZA NASI SASA

Tuwasiliane kwa Email: gmbongo.chuma@gmail.com

WE ARE HERE TO SERVE YOU

Keep you Entertained always

WE ARE HERE TO SERVE YOU

Habari na Burudani

WELCOME TO GMBONGO WORLD

Kwa habari za Burudani na zenye uhakika.

WAY

Friday, June 21, 2013

DIAMOND MUSICA ORIGINAL WAANDAA SHOW YA KUMKARIBISHA KING OF MELODIES CRISTIAN BELLA AMBAE ALIKUA NJE YA NCHI KWA MUDA MREFU KWA KAZI ZAKE BINAFSI KUSINDIKIZWA NA WAKALI BANANA ZORO NA DULLY SYKES

BAADA ya kukaa nje nchi kwa muda mrefu sasa cristian bella amerejea nchini tanzania ambapo karibu yake imeandaliwa show kabambe na bendi ambayo ni gumzo kwa sasa jijini dar ya DIAMOND MUSICA ORIGINAL iliyo chini ya LIVER HASSAN SULTANI ambapo kwa mujibu wa kiongozi huyo amesema wameamua kuandaa show kwa ajili ya cristiani bella ni kwa ajili ya kuonyesha ushirikiano na sio ya kwamba wanataka atue katika bendi yao ila ni utaratibu ambao amesema wameamua kufanya ili kukuza mziki wa dansi bongo ambao unasemekana unaelekea kupotea lakini anaamini kwa ushirikianona bendi nyingine basi muziki wa dansi utarudi kama zamani hivyo wamendaa show tatu ambazo watapiga na bleea huku show mbili wakijua watazifanya moja ndio itakua tar 28 pale MZALENDO PUB HUKU nyingine ikienda kufanyika pale MANGO GARDEN
AIDHA cristian bella atatambulisha nyimbo zake mpya mabazo zitakua katika album yake ya KING OF THE MELODIES ambayo itakua na takriban nyimbo nane

Thursday, June 20, 2013

SKYLIGHT BAND WANA CAROLINA KUDONDOSHA SHOW SPESHO IJUMAA HII NDANI YA TIE VILEGE USIKU WALIOUPA JINA LA USIKU WA MWAFRICA ATAKAVAA KIAFRICA ZAIDI KUZAWADIWA

AKIONGEA na blog hii kiongozi wa skylight band ANETH KUSHABA amesema ijuma hi wameamua kuifanya tofauti zaidi na kuwa kama zawadi kwa mashabiki wao wanaohudhuria kila siku na kuona mabadiliko zaidi katika show watakaoifanya siku hiyo ambayo itatawalia na nyimbo za kiafrica zaidi na mavazi ya kiafrica yatatawala usiku huo huku mshindi atakae vaa kiafrica zaidi kuzawadia na wanaskylight wenyewe,huku akisema lengo ni kukuza muziki wa kiafrica na utmaduni wa kiafrica zaidi ingawa amesema huo sio mwsho wa showkama izo zitakua nyingi tofauti tofauti na hii ikiwa ni kuboresha zaidi na kuwapa mashabiki wa bendi hiyo hamu ya kuendelea kuwa na kwa kufanya vitu tofautizaidi katika muziki wa live

Tuesday, June 18, 2013

BAADA YA KUWASHNGAZA WAZUNGU NCHINI FINLAND TOTOO ZE BINGWA ATUA BONGO NA ALBUM YAKE ALIYOIPA JINA LA ZERO HUKU AKISEMA NI ZAWADI KWA WATANZANIA LAKINI PIA ASEMA ATAFANYA SHOW NA AKUDO LAKINI SIO MAANA YA KWAMBA AMEREJEA TENA AKUDO

GWIJI la kurap katika miziki ya dansi totoo ze bingwa aliewahi kutamba na bendi kama vile BANA BETA,FM ACADEMIA,AKUDO IMPACT na sasa akiwa anamiliki bendi yake mwenyewe na kuipa jina la SANA SANAA BAND ambayo yuko na kina alain mulumba aliewah kutamba na diamond sound pamoja nakatanyama ingawa anasema kuwa pamoja na kuwa na watu hao ila wapo huru kuipigia bendi yoyote ile au kufanya kazi yoyote ile nje ya sanaa sana bendi lakini pindipo wanapopata show basi wanaweza kufanya pamoja.

AKIZUNGUMZIA festival aliyokwenda kufanya nchini finland amesema imekua ya mafaniko sana ni moja kati ya festila kubwa kabisa nchini humo ambapo pia ameweza kupiga show kadhaa katika mikoa ya lfinlnd naa kusema amesikia fahari ameiwakilisha vyema tananznia ingawa hakuweza kwenda na wanamuziki wake wote wa sanaa sana bendi alioenda nao na vile vile aliokutana nao huko waliweza kukutana na kufanya kitu kitu kimoja cha maana kilochoacha wazungu wakijiuliza
aidha pia toto amerejea na album yenye nyimbo nane huku akisema imefanyiwa mastering ya kimataifa na kusema copy nyingine ameziacha finland na copy nyingine amekujana nazo bongo soon ataanza kuzisambaza

Wednesday, June 12, 2013

SIKILIZA HAPA MWANAFALSAFA AKIFUNGUKA BIFU LAKE NA LADY JAY DEE NA KUSEMA WATU WANAJAJI BILA KUFIKIRI LAKINI PIA AIZUNGUMZIA SHOW YAKE YA TAR 14 LAKINI PIA VILE VILE SIKILIZA GADNER G HABASH AKIIZUNGUMZIA SHOW YA LADY JAY YA TAR 14 LAKINI JE UNAJUA LADY JAY NA MWANAFALSA NDIO WALIOFANYA COLABLE NYIMBO NYINGI ZAIDI SIKILIZA HAPA

Tuesday, June 11, 2013

BAADA YA TUZO ZOTE ZA BENDI KUELEKEA KWA MSHUJAA MUSICA BENDI LUIZA MBUTU AFUNGUKA NA KUSEMA HILO NI JAMBO LISILOWEZEKANA NI UCHAKACHUAJI WA HALI YA JUU INA MAANA HATA ALIPOCHUKUA YEYE ANGEKUWEPO MWANAMUZIKI WA MASHUJAA ANGECHUKUA ASEMA WAANDAJI WAJIPANGE TENA KUZINDUA ALBUM YAO NYUMBANI NI NYUMBANI MWISHO WA MWEZI

MSANII wa twanga pekee aliepokea tuzo ya band akiwa kama mwanamuziki bora wa kike wa muziki wa bendi ambe pia ni kiongozi wa twanga pepeta luiza nyoni mbutu amsema tuzo za mwaka huu zimejaa hujuma kiasi ambacho hawezi kuamini kuwa mashujaa musica wanaweza kuchukua tuzo zote za kili ni jambo lisilo wezekana ila kuna biashara iliyofanyika katikati ili kuikuza bendi lakini kuna categori nyingine hawastahili kupewa hata kwa akili ya haraka haraka huku akitolea mfano bendi bora ya mwaka lazima iwe haijapanguka kwa muda wa mwaka mzima lakini pia na hata uzoefu wa kuangalia show pindipo wanapoperfom inaonyesha kuwa hawawezi kuwa bendi bora ya mwaka na kusema kungekua na mwanamke mashujaa basi angeibuka kidedea jambo ambalo lingekua si kweli na hata kwenye categori aliechukua yeye tuzo imebidi watoe kwa sababu wameshindwa kuchakachua.
Aidha luiza amesema hayo yamepita na harakti zinaendelea kwa sasa wako mbioni kuzindua album yao ya kumi na tatu waliyoipa jina la NYUMBANI NI NYUMBANI ambapo itakua na nyimbo sita zilizotunga na
SHAMBA LA TWANGA( Greyson semsekwa)WALIMWENGU(j4)NGUMU KUMEZA(mirinda nyeusi)NYUMBANI NI NYUMBANI(kalala jounior) na nyingine mbili na huku akiongeza kuwa siku hiyo watazindua video za album yao pamoja na audio na watu wajue kuwa twanga pepeta itabaki kuwa twanga daima

Monday, June 10, 2013

CHALZ BABA SISITIZA KUWA KAZI NDIO NDIO ZILIZOFANYA MASHABIKI KUWACHAGUA KUWA WAO BORA KWA KILA KITU NA SIO UCHAKACHUAJI SASA KUANDAA MATAMASHA YA BURE KWA AJILI YA WANANCHI

Akiwa ameibuka na tuzo mbili za muimbaji bora wa mwaka wa bendi lakini mtunzi bora wa mashairi wa bendi lakini wakati huo huo wakiwa wamechukua wimbo bora wa mwaka wa bendi lakini pia bendi bora ya mwaka nikutokana kazi nzuri walioifanya kwa mwaka mzima katika album yao ya risasi kidole ambayo imepokelwa na mshabiki kwa wingi sana mpka kuipa kura bendi hiyo inayoundwa na wasanii mahiri akiwemo chalz baba mwenyewe lakini pamoja na rapa aliechukua tuzo kuwa rapa bora wa muziki wa bendi FURGUSON na kusema kuwa kazi yao ndio imewafanya hivyo sio wale waliokaa mwaka mzima nyumbani
akizungumza na mm meneja wao bw martini soppter amefunguka na kusema kuwa kwa sasa wanaanda matamsha ya bure sehemu mbalimbali ili kutoa shukuran zao kwa wadau waliowawezesha kuwapigia kura


Wednesday, June 5, 2013

HIVI NDIVYO ILIVYOKUA MISS MTWARA REGION MWAKA 2013 AMBAPO MWANADADA YVONE STEVEN ALIIBUKA KIDEDEA

                                HAYA NDIO BAADHI YA MATUKIO KATIKA KINYANG'ANYIRO CHA         KUMSAKA MLIMBWENDE WA MKOA WA   MTWARA



















.

.

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...