WELCOME TO GMBONGO BLOG

To keep the body in good health is a duty... otherwise we shall not be able to keep our mind strong and clear.

TANGAZA NASI SASA

Tuwasiliane kwa Email: gmbongo.chuma@gmail.com

WE ARE HERE TO SERVE YOU

Keep you Entertained always

WE ARE HERE TO SERVE YOU

Habari na Burudani

WELCOME TO GMBONGO WORLD

Kwa habari za Burudani na zenye uhakika.

WAY

Friday, September 30, 2011

HUKU NDIKO ALIKOTOKA KAMARADE ALLY CHOKI MKURUGENZI WA EXTRA BONGO

    LE KAMARADE ALLY CHOKI A.K.A KIBABU CHA LOLIONDO
 Alizaliwa miaka 41 katika mkoa wa pwani wilaya ya kibaha na kupatia elimu yake ya msingi akiwa ameipatia mkoa huo huo wa kibaha lakin kwa asili ni mwenyeji wa kusini mwa Tanzania
 LE KAMARADE ALLY CHOKI alianza kujingiza katika tasnia ya muziki rasmi mnamo mwaka 1987 na band ya sehemu alikokulia ye mwenyewe anasema band ya kimtaa kipindi hicho ikiitwa KIBAHA SOUND kipindi hicho akiwa na mtu mmoja akiitwa  SHOMARI MGUTA alikaa katika band hiyo ya kibaha sound kwa mwaka mmoja tu baadae
   Mwaka 1988 alihamia jiji Dar-es-salaam na kutua katika band moja iliokua na masknai yake pale manzese darajini kipindi hicho hakuna daraja na ni band inayosemeka imeibua vipaji vya wasanii wengi waliowika mwanzoni miaka yaelfu mbili kama kina YAHAYA MKANGO,MUUMINI MWINJUMA kipindi hicho band hiyo ikiitwa LOLA AFRICA ambapo alikua na mkongwe FRANCIS LUBUA NA YAHAYA MKANGO huku kipindi hicho wakipiga miondoko ya kiafrica
 kama JAZZ,RHUMBA,DANCE na miondoko mingine ya kiafrica lakini mara nyingi sana walikua wakipiga copy ambapo alidumu kwa muda wa mwaka mmoja tu.
 Mwaka 1989 alihamia katika band ya MWENGE JAZZ iliyokua na maskani yake mwenge ambapo hapo ally alikaa muda wa kama miezi sita hivi ndipo alipochomoka na kwenda kuwa mmoja kati ya waasisi wa bad inayotikisa hadi sasa ambapo wengi wanadhani muasisi wa band hiyo ni KOMANDOO HAMZA KALA lakini La wanzilishi wa band ya BANTU GROUP ya kwanza walikua ni kina ALLY CHOKI,BUSEMBA AMINYUGU,ATHMAN MANGELESANGE,PETER PATII,RASHID KALALA,MUHANDO ambapo hapo akiwa na wana bantu group alifanikiwa kutunga kibao kilicho mtambulisha katika ramani ya muziki wa dansi kipindi hicho cha BABA JANE na waliweza kutoa album liyobeba jina hili, kama miaka miwili hivi ilitosha kujenga jina la bantu group kwake
 Mwaka 1991 alitoka batu na kujiunga na band ya LEGO STAR lakini hakudumu sana kwa kuwa nyumbani ni nyumbani ilibadi
 1992c arejee tena BANTU GROUP ambapo hapo sasa ndipo alipomkuta KOMANDOO HAMZA KALALA na aliweza kuibuka tena na kibao cha BABA JANE No 2,MKANDA WA MAPENZI wakati huo hasimu wake wa kipindi cha miaka ya 2000 MUUMIN MWINJUMA alikua nae katika bantu group ilimtosha miezi kadhaa tu mwaka huo huo alihamia band nyingine ikiitwa MK BEATS ambapo alimalizia miezi 6 na
  
                                         ALLY CHOKI NA BANZA STONE

Mwaka 1993 alijunga na band ya WASHIRIKA maarufu kipindi hicho kama WATU NJATA NJATA hapo alijiunga na kina ZAHIR ALLY ZORRO,MAREHEM ADAM BAKARI,MAREHEM TOPHY MBAMBE,EMA KELO mke wa edy shege ambapo hapo walikua hatari sana na aliweza kuibuka na nyimbo kama GUBU LA WIFI,USHOGA UKIZIDI,RED CHAMPION,MAMA ELIZA vyote hivyo hata mwaka hakumaliza
 Hiyo hiyo 1993 alirudi tena nyumbani bantu group alikutana na bonge ya tour kwenda UFARANSA,DERNMARK,SWEEDEN
 Lakini walivyorejea tu mwaka 1994 alitua moja kwa moja pale nchini KENYA katika jiji la Nairobi ambapo waliweza kuunda kundi moja waliloliita bongo ngoma kama mwaka mmoja hivi
 1995 ndipo jeshi la kenya lilikua na Band yake ndipo alipoibukia tena kamarade ALLY CHOKI na kama watu wengi walivyokua hawajui basi kibao cha JIRANI original alikitunga akiwa kule kabla kuja kurejea tena na band ya kitanzania miaka ya 2000 ila alitunga nyingine ya MTOTO MKIWA,NAIPENDA KENYA labda kama huji tu hapo katika band hiyo ALLY ndio alikua mtanzania pekee wengine wote kutoka kenya lakini mwaka huo huo alihamia  kisumu huko huko nchini kenya na kuanzisha band nyengine ya watanzania kiipindi hicho akiwa na ROGGERT HEGGA,KING JOBISO,KING  KONG,EPHRAIM JOSHUA,NA MAREHEM KOMBO MSICHOKE.
                                  LE KAMARADE ALLY CHOKI ENZI HIZO


                                        ALLY CHOKI
Mwishoni mwa mwaka 1999 alitua katika kundi la african stars na kuwakuta watu kama AMIGOLASO,LUIZA NYONI,JESCA CHALS,BANZA STONE, na mwaka mmoja babadae baada ya kuondoka kwa banza stone ndipo alipofanikiwa kuurudia wimbo wa JIRANI ambayo alikua ameuanza nchini kenya na kutengeneza album iliyobeba jina hilo huku ndani kukiwa na nyimbo nyingine ya LIGHTENESS  ikiwa ni utunzi wake mwenyewe
mkwa 20001 ikiwa na african stars FAINALI UZEENI,2002-CHUKI BINAFSI,2003 UKUBWA JIWE  ambapo alikua na nyimbo nyingine iliyotamba sana kipindi hicho ya WALIMWENGU NO 01
Lakini mwaka 2004 aling'atuka african stars na kwenda kuanzisha band yake mwenyewe iliyoitwa EXTRA BONGO 3*3 ambapo aliwaibuwa watu kama kina RICH MAARIFA,BASHIR UHADI,GREYSON SEMSEKWA,BONZO KWEMBE KHALID CHOKORAA na wengine kibao hapo aliweza kufyatua album walioipa jina la 3*3 huku ndani kukiwa na nyimbo kama BULLET PROOF,DUBLE DUBLE
 Mwaka 2005 waliweza kuanzisha band nyingine ambayo ilitoka katika band mbili tofauti EXTRA BONGO NA DOUBLE M na kuunda kundi la DOUBLE EXTRA akiwa yeye pamoja na MUUMIN MWINJUMA
 Na walitoa album moja ya NDOA

  KHADIJA MNOGA,ALLY CHOKI,BANZA STONE, MUUMINI MWINJUMA
Mwaka 2005 alitua katika band ya MCHINGA GENERATION au G.8 ambapo aliweza kusaidia kufyatua albam ya MWAKA WA TABU,KILA CHENYE MWANZO,NGUZO TANO ZA MAPENZI.
 Mwaka 2006 alirejea tena TWANGA PEPETA AFRICAN STARS ambapo mwaka 2007 alibuka na nyimbo kama PASSWORD iliyobeba jina la album FURAHA YA HARUSI,ALL EYES ON ME.
2007-nyimbo ya MTAA WA KWANZA iliyobeba jina la album na UVUMILIVU
 2008 -Alitua tena T.O.T RESPECT lakini hapo hakuweza kufyatua album yeyote
Mwaka 2009 mwezi wa 6 alirudisha tena EXTRA BONGO saari hii akija na slogan ya NEXT LEVEL ambapo tayari washafyatua album iliyotikisa mji ya MJINI MIPANGO huku kukiwa na nyimbo ya rhumba ya FIRST LADY
 NA mwaka 2011 amefanyia mabadiliko kundi lake hilo la EXTRA BONGO na sasa wako mbioni kufyatua album ambayo nyimbo zake zipo tayari kasoro kuchagua jina la album.


 HUYO NDIO LE KAMARADE ALLY CHOKI .ak.a MZEE WA KIJIKO a.k.a MZEE WA FARASI a.k.a KIBABU CHA LOLIONDO.

Wednesday, September 28, 2011

KAA TAYARI KWA KUNDI JIPYA LA TAARABU LENYE WASANII LUKUKI WENYE VIPAJI


                NI T MOTO MORDEN TAARAB
Ni kundi jipya lenye vipaji vingi katika makundi ya taarab yanayochipukia kwa kasi katika ulimwengu wa muziki wa mwambao, ni kundi ambalo liantarajiwa kuzinduliwa rasmi siku ya ijumaa ya tar 28.10.2011
     TANZANIA MOTO MORDEN TAARAB inaundwa na sheni ya wanamuziki wakali akiwemo JOKHA KASIM,SABIHA MAGUMASHI,AISHA MASANJA, BI MWANAHAWA,YOUNG HASSAN ALLY,HANIPHER JUMA,na aliewahi kuwika katika mashindano ya BONGO STAR SEARCH, MRISHO RAJABU,MOSI SULEIMAN na wengine kibao

                                   BI. MWANAHAWA ALLY MZIGONI NA T.MOTO MORDEN TAARAB
Kwa habari za kuamika kuwa kundi la T MOTO TAARAB litazindua album mbili kali huku moja itabeba jina la ALIENIUMBA HAJANIKOSEA ulioimbwa na gwiji na mkongwe wa muziki wa taarabu B. MWANAHAWA ALLY ambao wengi wanaweza kumkumbuka kwa KINYAGO CHA MPAPURE, na nyingine nyingi zilizo tamba sana kipindi hicho, vilevile T MOTO ina mkali JOKHA KASIMU ambae kibao alicho kiiimba ndani ya T MOTO kishaanza kutikisa jiji na nchi kwa ujumla kwa wapenda muziki wa mwambao UNAVYOJIDHANI HAUFANANI.

                    JOKHA KASSIM MOJA KATI YA WAKALI WA T MOTO MORDEN TAARAB
Kwa mujibu wa mzee katumba kwa kuanza wataanza na nyimbo kibao na akizitaja nyimbo zitakazo kuwepo kwenye album hiyo ni pamoja na ALIYENIUMBA HAJANIKOSEA iliyoibwa na Bi.Mwanahawa ally UNAVYOJIDHANI HAUFANANI-Jokha kassim,RIZIKI SHORTCUT-Aisha masanja,TOP BONGO-Young Hassan Ally MCHIMBA KABURI SASA ZAMU YAKE-Mrisho Rajabu,UMESUSA TEMBELE HELA YA NYAMA UNAYO-Shinuna kassim pamoja na NIPO SIMPLE-Mosi suleyman
           MKALI SABIHA MAGUMASHI AKITA VOCAL KATIKA KALI ZA T MOTO.
                YOUNG HASSAN ALLY AKIFANYA KWELI NDANI YA TOP BONGO
  MRISHO RAJAB NDANI YA MCHIMBA KABURI SASA ZAMU YAKE.......

                          TANZANIA MOTO MORDEN TAARAB   (T.MOTO TAARAB)
             JOKHA KASSIM NDANI YA T MOTO NA UNAVYOJIDHANI HAUFANANI

             AMIN SALMIN MKURUGENZI WA T- MOTO MORDEN TAARAB
    SASA KAA MKAO WA KULA KUPOKEA VITU VIKALI KUTOKA T.MOTO TAARAB
                       HAPANA CHEZEA UTAUNGUA

Monday, September 12, 2011

UNAKATA KUFAHAMU WASIFU WA WANAMUZIKI WA MUZIKI WA DANSI TANZANIA TOKA WALIPOANZIA MPAKA WALIPO SASA?

Baada ya kuona wanamuziki wengi wa muziki wa dansi kupotea bila ya kujulikana wasifu wao walipoanzia mpaka walipo sasa na hivo kufanya kwa kuwafanya wanamuziki wa dansi wa sasa wakumbukwe duniani kote basi G.MBONGO THA INTERTAINER katika mfululizo wa wasifu au wengi wamezoea kwa jina la kingereza profile za wanamuziki wa band mbali mbali zinazotamba TANZANIA hii ni katika kuhakikisha wasanii wa muziki wa dansi hawapotei kama waliopotea miaka ya nyuma nikiwa kama shabiki namba moja wa muziki wa kiafrica nakuahidi kuanzia wiki hii utakuwa unapata update za muziki wa dansi na ratiba zao vile vile habari zao kupitia blog hii thanks kwa wasanii wote ambao wanashow love na mimi na kuweza kufanikisha hili nalotaka kulifanya kwa ajili ya muziki wa dansi tanzania follow ma back aluta continue vuallaaaaaa
 hapana chezea G.MBONGO TOLEKAAAAAAAAAAAA!

.

.

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...