WELCOME TO GMBONGO BLOG

To keep the body in good health is a duty... otherwise we shall not be able to keep our mind strong and clear.

TANGAZA NASI SASA

Tuwasiliane kwa Email: gmbongo.chuma@gmail.com

WE ARE HERE TO SERVE YOU

Keep you Entertained always

WE ARE HERE TO SERVE YOU

Habari na Burudani

WELCOME TO GMBONGO WORLD

Kwa habari za Burudani na zenye uhakika.

WAY

Wednesday, April 8, 2015

MADEREVA WA VYOMBO VYA MOTO WATISHIA KUGOMA IJUMAA KWA MADAI YA KUFANYIA UNYANYASAJI

   Mabasi ya Abiria yakiwa yamepaki stand kusubiri

Madereva wa vyombo mbali mbali vya moto nchini Tanzania, wanakusudia kushiriki mgomo wa nchi nzima siku ya Ijumaa wiki hii, kuishinikiza serikali kuondoa kero mbali mbali zinazowakabili ikiwemo ukosefu wa ajira za uhakika pamoja na agizo la kutaka madereva hao waende kusoma kila wanapotaka kuhuisha leseni zao za udereva.

Wakizungumza kupitia Katibu wa Muungano wa vyama vya Madereva Bw. Rashid Saleh, madereva hao wamesema kuwa suala la kurudia kusoma ni aina nyingine ya unyanyasaji kwa maelfu ya madereva nchini, ambao kwa kipindi kirefu wamekuwa hawana mfumo mzuri wa ajira licha ya kutupiwa lawama kibao kuwa wao ndio chanzo cha ongezeko la ajali nchini.

Katibu huyo wa Muungano wa Vyama vya Madereva ameitaja kero nyingine kuwa ni hatua ya Chuo cha Taifa cha Usafirishaji NIT kutamka hadharani kuwa vyeti walivyonavyo madereva hao sio halali na kwamba Ijumaa wiki hii wanakusudia kukutana na Waziri wa Kazi na Ajira kwa ajili ya kuzungumzia kero hizo kwa lengo la kuepusha kutokea kwa mgomo huo.

Monday, March 30, 2015

MUGABE AWATAKA VIONGZI WA AFRIKA KUACHA KUWA VIBARAKA WA MATAIFA YA ULAYA NA MAGHARIBI NA WAJISHUGHULISHE KUINUA WANANCHI WAO



     Rais wa Zimbawe na Mwenyekiti wa umoja wa Africa Robert Gabriel Mugabe
Rais wa Zimbawe na Mwenyekiti wa umoja wa Africa Robert Gabriel Mugabe amewataka viongozi wa nchi za Africa kukataa kuwa vibaraka wa mataifa tajiri duniani na badala yake wajitoe katika kuwatumikia waafrika ili kufikia mafanikio ya kimaendeleo katika ustawi wa bara hili.

Rais Mugabe ametoa mwito huo wakati akizungumza katika mkutano wa kimataifa wa viongozi Vijana kutoka nchi mbalimbali za Bara la Afrika na China unaofanyika katika ukumbi wa mikotano wa Ngurdoto nje kidogo ya Jiji la Arusha.

Katika hotuba yake ya ufunguzi wa Mkutano huo Rais Mugabe ametumia muda mwingi kuwaasa na kutoa mwito kwa viongozi hao vijana akisistiza kuwa Bara la Afrika linategemea mchango wa Fikra zinazojali uwajibikaji na nidhamu ya hali ya juu katika utumishi.

Awali akizungumza katika Mkutano huo,Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dakta Jakaya Kikwete ameonyesha imani aliyoanayo kupitia mkutano wa viongozi vijana kutoka Afrika na Uchina kwamba utatoa fursa ya kutoka na maazimio yatakayokuwa na tija kwa mustakabali wa watu wote

Tuesday, March 24, 2015

SERIKALI KUTUNGA CHOMBO CHA KUCHUNGUZA, KUPEKUA NA KUKAMATA WATUHUMIWA WA MADAWA YA KULEVYA


            Waziri wa nchi ofisi ya waziri mkuu sera, uratibu na bunge Mh. Jenista Mhagama
Serikali leo imewasilisha mswada wa sheria ya kudhibiti na kupambana na dawa za Kulevya ya mwaka 2014, kutokana na tatizo hilo kuongezeka zaidi kuanzia mwanzoni mwa miaka ya 1980 na kutishia uhai wa taifa kutokana na vijana wengi kujiingiza katika biashara na matumizi ya dawa hizo.

Akiwasilisha mswada huo Waziri wa nchi ofisi ya waziri mkuu sera, uratibu na bunge Mh. Jenista Mhagama amesema matumizi ya dawa za kulevya yameongezeka ambapo takwimu zinaonyesha kuwa watumiaji wa dawa hizo kati ya laki mbili na 20 hadi laki nne na 20 hapa nchini wengi wakiwa ni vijana kati ya miaka 15 hadi 38.

Mh. Mhagama amesema ili kurekebisha matatizo ya kimfumo katika udhibiti ya dawa hizo serikali imekusudia kuanzisha chombo kinachojitegemea chenye mamlaka ya kiutendaji ya kuchunguza, kupekua na kukamata watuhumiwa tofauti na ilivyo tume kwa sasa.

Friday, March 6, 2015

WASHIKILIWA NA JESHI LA POLISI KWA KUWAUA WATU WATANO KWA KUWATUHUMU WACHAWI


     Kamanda wa Jeshi la Polisi mkoani Mara, Philip Kalangi akizungumza na wanahabari
Jeshi la polisi mkoa wa mara limewakamata watu saba wakiwemo viongozi wawili wa serikali ya kijij cha park nyigoti katika kata ya ikoma wilayani serengeti mkoani mara baada ya kutuhumiwa kuwakamata na kuwafunga vitambaa usoni watu wanane wanaowatuhumu kwa uchawi kisha kuwachapa viboko na kusababisha vifo vya watu watano.

Kaimu kamanda wa polisi mkoa wa mara,kamishina msaidizi wa jeshi la polisi Acp Ernest Kimola,amesema katika tukio hilo ambalo limesababisha watu wengine watatu kujeruhiwa kwa kuchapwa viboko hivyo na kulazwa katika hospitali teule ya nyerere ddh mjini mugumu wilayani serengeti.

Mbali na mwenyekiti na mtendaji wa serikali ya kijiji hicho kukamatwa pia viongozi wawili wa jadi wamekamatwa wakihusishwa na mauaji hayo

nao baadhi ya ndugu wa marehemu wameelezea jinsi unyama huo ulivyotekelezwa kwa kisingizio cha ushirikinai

hadi sasa askari wa jeshi la polisi kutoka makao makuu ya mkoa wa mara kwa kushirina na polisi mjini wilayani serengeti wanaendesha na operesheni kali katika kuwasaka watu wote walihusika kufanya mauaji hayo ya kinyama.

.

.

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...