WAY

Friday, March 6, 2015

WASHIKILIWA NA JESHI LA POLISI KWA KUWAUA WATU WATANO KWA KUWATUHUMU WACHAWI


     Kamanda wa Jeshi la Polisi mkoani Mara, Philip Kalangi akizungumza na wanahabari
Jeshi la polisi mkoa wa mara limewakamata watu saba wakiwemo viongozi wawili wa serikali ya kijij cha park nyigoti katika kata ya ikoma wilayani serengeti mkoani mara baada ya kutuhumiwa kuwakamata na kuwafunga vitambaa usoni watu wanane wanaowatuhumu kwa uchawi kisha kuwachapa viboko na kusababisha vifo vya watu watano.

Kaimu kamanda wa polisi mkoa wa mara,kamishina msaidizi wa jeshi la polisi Acp Ernest Kimola,amesema katika tukio hilo ambalo limesababisha watu wengine watatu kujeruhiwa kwa kuchapwa viboko hivyo na kulazwa katika hospitali teule ya nyerere ddh mjini mugumu wilayani serengeti.

Mbali na mwenyekiti na mtendaji wa serikali ya kijiji hicho kukamatwa pia viongozi wawili wa jadi wamekamatwa wakihusishwa na mauaji hayo

nao baadhi ya ndugu wa marehemu wameelezea jinsi unyama huo ulivyotekelezwa kwa kisingizio cha ushirikinai

hadi sasa askari wa jeshi la polisi kutoka makao makuu ya mkoa wa mara kwa kushirina na polisi mjini wilayani serengeti wanaendesha na operesheni kali katika kuwasaka watu wote walihusika kufanya mauaji hayo ya kinyama.

0 comments:

Post a Comment

.

.

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...