WAY

Monday, March 2, 2015

ETI TANESCO WAMESEMA WATALETA MFUMO MWINGINE WA KUNUNUA LUKU BAADA YA TATIZO LA MITANDAO KUKOSA NETWORK YA KUNUNUA UMEME

Meneja Mawasiliano wa Tanesco Adrian Mvungi
Wakazi na wajasiriamali wa jiji la Dar es salaam wamelilalamikia Shirika la Ugavi wa Umeme nchini Tanesco baada ya Mtandao wa kuuza umeme kwa njia ya Luku kugoma kufanya kazi toka juzi usiku,

Wakizungumzana kutoka makao makuu ya Tanesco Ubungo jijini Dar es salam huku wakiwa na jazba wamesema biashara zao zimehathirika sana na kuwa sababishia hasara kutokana na kushindwa kununua Umeme kwa njia ya Luku huku biashara zao zikitegemea umeme wakati wote,

Kwa Upande wake Meneja mwandamizi Teknolojia ya Habari na mawasiliano wa Tanesco Kusenha A. mazengo amesema wamelifanyia kazi tatizo hilo na kuhaidi hivi karibuni wataleta mfumo mpya wenye njia mbadala wa kununua Umeme,

Wakati huo huo Meneja Mawasiliano wa Tanesco Adrian Mvungi amewaomba radhi wateja wao kwa usumbufu walioupata na kuhaidi kutorudia tena.

0 comments:

Post a Comment

.

.

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...