WAY

Tuesday, March 24, 2015

SERIKALI KUTUNGA CHOMBO CHA KUCHUNGUZA, KUPEKUA NA KUKAMATA WATUHUMIWA WA MADAWA YA KULEVYA


            Waziri wa nchi ofisi ya waziri mkuu sera, uratibu na bunge Mh. Jenista Mhagama
Serikali leo imewasilisha mswada wa sheria ya kudhibiti na kupambana na dawa za Kulevya ya mwaka 2014, kutokana na tatizo hilo kuongezeka zaidi kuanzia mwanzoni mwa miaka ya 1980 na kutishia uhai wa taifa kutokana na vijana wengi kujiingiza katika biashara na matumizi ya dawa hizo.

Akiwasilisha mswada huo Waziri wa nchi ofisi ya waziri mkuu sera, uratibu na bunge Mh. Jenista Mhagama amesema matumizi ya dawa za kulevya yameongezeka ambapo takwimu zinaonyesha kuwa watumiaji wa dawa hizo kati ya laki mbili na 20 hadi laki nne na 20 hapa nchini wengi wakiwa ni vijana kati ya miaka 15 hadi 38.

Mh. Mhagama amesema ili kurekebisha matatizo ya kimfumo katika udhibiti ya dawa hizo serikali imekusudia kuanzisha chombo kinachojitegemea chenye mamlaka ya kiutendaji ya kuchunguza, kupekua na kukamata watuhumiwa tofauti na ilivyo tume kwa sasa.

0 comments:

Post a Comment

.

.

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...