WAY

Wednesday, November 13, 2013

MWENYEKITI WA NCCR MAGEUZI ATOA RATIBA YA MAZISHI YA DK SENGODO MVUNGI JESHI LA POLISI LASEMA LINAWASHIKILIA WATU TISA KUHUSIANA NA TUKIO HILO

Mkurugenzi wa Katiba, Sheria na Haki za Binadamu wa NCCR-Mageuzi, Dk Sengodo Mvungi amefariki dunia jana alasiri nchini Afrika Kusini alipokuwa akipatiwa matibabu.

Taarifa za kifo chake zimethibitishwa na Mwenyekiti Taifa wa NCCR-Mageuzi, James Mbatia.

Akizungumuza na safari radio leo asubuhi Mbatia amesema taratibu za mazishi zimekwishapangwa ambapo mwili wa marehemu utawasili nchini siku ya ijumaa ya tar 15 na kusomewa ibada tar 16 katika kanisa la mt joseph jijini Dar-es-salaam

Aidha siku hiyo hiyo  saa 9 na nusu utapelekwa karimjee kwa ajili ya kupewa heshima za mwisho na viongozi pamoja na watu mbalimbali.

Mbatia ameongeza kuwa jumapili ya tar 17 jioni mwili utasafirishwa kupelekwa mkoani Kilimanjaro katika wilaya ya mwanga kwa ajili ya maziko yatakayofanyika tar 18.

Dk Mvungi alijeruhiwa kwa kukatwa na mapanga kichwani Novemba 13, mwaka huu nyumbani kwake Kibamba Msakuzi na watu wanaosadikiwa ni majambazi.

Hati hivyo jeshi la polisi linawashikilia watu tisa kutokana na tukio hilo la lililopelekea kifo cha mwanaharakati huyo

Waziri wa mambo ya nchi dk nchimbo alitoa ripoti hiyo juzi na kusema watu wate waliokamatwa walikiri kuhusika na tukio hilok kwa kuwa walikutwa na mapanga yenye damu simu ya nokia inayosemekana iliibiwa siku ya tukio

watu wanaosadikiwa ni majambazi walimvamia dk mvungi nyumbani kwake kibamba na kumkata na mapanga kisha kutoweka.

mungu ailaze roho ya marehemu mahala pema peponi amin 



 

0 comments:

Post a Comment

.

.

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...