WAY

Tuesday, February 18, 2014

KAMATI kuu ya chama cha mpainduzi - CCM –imewapa onyo kali viongozi sita wa chama hicho kufuatia kubainika na tuhuma mbalimbali zikiwemo za kukiuka maadili ndani na nje ya chama hicho.



KAMATI   kuu  ya chama  cha mpainduzi - CCM –imewapa  onyo  kali    viongozi  sita wa  chama  hicho  kufuatia kubainika na tuhuma  mbalimbali  zikiwemo za   kukiuka  maadili   ndani na nje ya  chama hicho.

Hatua hiyo  imekuja baada ya kamati hiyo  kukutana  na viongozi hao na kuwahoji juu ya tuhuma hizo  na baada ya kuhojiwa  walibainika kuwa tuhuma hizo ni za kweli.

Hayo  yamebainishwa  leo  jijini  Dar es Salaam  na  Katibu  wa  halmashauri  kuu  ya taifa ,  itikadi  na uenezi  Nape  Nnauye wakati alipokuwa  akizungumza na waandishi wa  habari  kuhusiana   vikao  vya pamoja vilivyofikiwa  na kamati  kuu,   tume ya  udhibiti  na nidhamu na  kamati  ndogo ya udhibiti.

Amesema  kuwa  kwa mujibu wa kanuni za uongozi  na maadili  za CCM  toleo la  februari  2010 ibara  ya nane na  kuongeza  kuwa  tuhuma hizo  zilizobainika zinaukweli  ndani yake  hivyo  kupelekea  mapendekezo  hayo  kwenye  tume  ya udhibiti  na nidhau.
Amewata  viongozi hao  waliopewa  onyo  kuwa  ni Fredick Sumaye, Edward Lowassa, Stephano Wasira,  Benard  Membe , Januari  Makamba na Wiliam  Ngeleja.

Aidha   ameyataja  makosa  yao  kuwani ni  kuthibitika  kuanza  kampeni  za kuteuliwa   kugombea nafasi ya urais kabla  vya  wakati wake jambo   ambalo  ni kinyume  na kanuni  za uongozi  n  maadili  za  chama  hivho.

 18-FEBR-NAPE NNAUYE
Pia  amesema kuwa  mwanachama  aliyepewa  adhabu  ya onyo kali  atakuwa  katika  hali  ya  kuchunguzwa  kwa muda  wa  usiopungua  miezi  12  ili  kumsaidia  katika jitihada  za kujirekebisha.


0 comments:

Post a Comment

.

.

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...