WAY

Friday, February 21, 2014

WAKIWA WANAELEKEA KWENYE UZINDUZI WA MTENDA AKITENDEWA KESHO ALLY CHOKI AFUNGUKA KUHUSU REDOCK MAUZO NA KABATANO ASEMA HAJAFANYA LOLOTE NDANI YA EXTRA BONGO NA HAWEZI KUWAZUNGUMZIA ASEMA NI WATU WASIOKUMBUKA FADHILA TAMAA ZA PESA ZA MARA MOJA NDIO ZIMEWAPONZA ASEMA SASA TIMU ALIYONAYO NDIO KIKOSI CHA MAANGAMIZI WATU WASUBIRI SUPRISE KWENYE UZINDUZI KAMA KAWAIDA YAKE

Mkurugenzi wa extra bongo nextlevel LE KAMARADE ALLY CHOKI MZEE WA KIJIKO IGWEE amefunguka kuhusiana na sakata la wanamuziki waliondoka kwenye band yake na kwenda kufanya show za nje bila ruhusa yake ingawa wao wanasema aliwaruhusu ila dakika za mwisho ndio akawakatalia kwanza kabisa choki alisema hawezi kuongea kuhusu kabatano kwa sababu hakuna kikubwa alichokifanya extra bongo kwa hivyo hata akiondioka hakuna kitakacho haribika ila amesema tamaa ndio imewapoza lakini pia wanasahau fadhila kwa sasa walikotoka katika band walioenda kuifanyia kazi walishwahi hata kutiwa ndani lakini ally choki ndio aliweza kuwasaidia na leo ndio wanaona sehemu nzuri ya kwenda kufanya kazi na pia ameongeza pia alishwapa taarifa toka awali kuwa wasiende katika hilo onyesho lakini mwisho wa siku waka kaidi amri yake na ndio mwisho wa siku akaamua aliyoaamua na ndipo alipofikiria kumchukua GREYSON SEMSEKWA kuweza kusaidiana nae katika sehemu za kurap na gery ni mmoja kati ya watu wa mwanzo sana ndani ya extra bongo.


Aidha ally choki amesema kuchelewa kwa uzinduzi huo kulitokana na kukamilisha viedo kwanza lakini na pia kutambua wanamuziki wa kweli ambao anaweza kufanya nao kazi kwa muda mrefu
Amezitaja nyimbo atakazokwenda kuzindua nazo kesho ni pamoja na MTENDA AKITENDEWA,WATU NA FALSAFA,BAKUTUKA,UFISADI WA MAPENZI,MAMA SHUU,NEEMA ambazo zilikuwa zimekamilika toka mwaka jana na pia amesema siku hiyo atasindikizwa na wasanii wengi akiwemo KHADIJA KOPA,AMINI,LINAH,MASHUJAA MUSICA band na itakua ndani ya ukumbi wa dar- live mbagala

0 comments:

Post a Comment

.

.

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...