WAY

Tuesday, February 18, 2014

WASANII nchini wametakiwa kujiunga katika mfuko wa pesheni kwa watumishi wa umma –PSPF-ili waweze kujiwekea akiba kwa maaisha yao ya baadae.

2

WASANII nchini wametakiwa  kujiunga  katika  mfuko wa  pesheni  kwa watumishi wa  umma –PSPF-ili  waweze  kujiwekea  akiba kwa maaisha  yao  ya  baadae.

Hayo  yamesemwa leo  jijini Dar es Salaam na  Meneja  msaidizi  mpango  wa uchangiaji wa hiari –PSPF-Matilda  Nyallu wakati alipokuwa akizungumza na waandishi wa  habari  kuhusiana na  semina  ya wasanii  hao  inayotarajiwa  kufanyika  februari 21  mwaka  huu.

Matilda  amesema kuwa   katika  semina hivyo  ambayo  wataitoa kwa wasanii   inalengo la  kuwashawishi  kujiwekea  akiba  ambayo  itamsaidia  kwa baadae kwa sababu  asilimia kubwa ya wasanii  hawana  akiba ya  baadae.

Amesema kuwa  kabla  ya  kuwashawishi kujiunga  na mfuko huo  watatoa  elimu   ili  waweze kuelewa   kwa  undani umuhimu wa  kujiwekea akiba.

Kwa  upande  wake  Mwenyekiti wa  bongo  movie Stivu  Nyerere  amesema kuwa kinachotakiwa  wasanii wajitambue pamoja na  kuitaka  serikali iweke  sheria  kali  kwa  watu  wanaoiba  kazi  za wasanii kwa sababu   wanachangia kurudisha  nyuma  maendeleo  ya  wasanii.

Aidha  amewataka wasanii  wa hapa  nchini  waungane kwa  pamoja na  kupinga  hatua  ya  kuuza hati miliki  ya kazi  zao kwa  sababu  zinachangia kwa  asilimia kubwa  kukosa haki zao za msingi  za  kazi  wanazofanya

0 comments:

Post a Comment

.

.

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...