WAY

Wednesday, August 6, 2014

JUKWAA LA KATIBA LASIKITISHWA NA BUNGE MAALUMU LA KATIBA KUANZA BILA UKAWA


                               Deus Kibamba
Jukwaa la katiba nchini Tanzania limesikitishwa na namna Bunge Maalumu la Katiba linavyotaka kunyamazisha sauti na mijadala ya wananchi, kuhusu kasoro zinazojitokeza katika mchakato unaoendelea wa kutafuta katiba mpya.

Mwenyekiti wa Jukwaa hilo Bw. Deus Kibamba ametoa kauli hiyo jana wakati akiongea na East Africa Radio jijini Dar es Salaam, ikiwa ni siku moja tangu kuanza kwa vikao vya bunge maalumu la katiba ambapo baadhi ya wajumbe wa bunge hilo wamenukuliwa wakiitaka serikali izuie midahalo ya wazi kuhusu mchakato wa katiba mpya

Aidha, Kibamba amesema mwishoni mwa juma hili Baraza la Vyama vya Siasa litakutana na pande hasimu katika mchakato wa katiba, ikiwa ni sehemu ya harakati za kupatanisha pande hizo, katika kile alichoeleza kuwa ni fursa pekee na ya mwisho ya kunusuru mchakato huo dhidi ya hatari ya kuvunjika.


0 comments:

Post a Comment

.

.

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...