WAY

Monday, November 3, 2014

BAWACHA WALAANI VIKALI VURUGU KWENYE MJADALA WA JAJI WARIOBA



                          Mwenyekiti wa Baraza la Wanawake CHADEMA, Halima Mdee
Baraza la Wanawake wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA, nchini Tanzania limelaani vikali Vurugu alizofanyiwa aliekuwa Mwenyekiti wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba Jaji Joseph Warioba zilizotokea hivi karibuni.

Akizungumza katika Mkutano wa Hadhara katika Ziara ya Baraza hilo kanda ya Ziwa Mwenyekiti wa BAWACHA, Mh. Halima Mdee amesema kitendo alichofanyiwa Jaji Warioba ambae alishika Nyadhifa za Juu serikalini Hakikubaliki.

Mh. Mdee pia Vijana wa Chama hicho Mkoa wa Dar es Salaam waepuke kujiingiza katika vurugu kama hizo ambazo zinahatarisha amani ya nchini na kusema wao kama Chama watazunguka nchini nzima kuendelea kutoa Elimu kuhusu kupinga katiba inayopendekezwa na Kujiandikisha ili kupiga kura katika Chaguzi za Serikali za Mitaa.


0 comments:

Post a Comment

.

.

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...