WAY

Tuesday, November 4, 2014

VIJANA WATAKIWA KUACHA KUTUMIKA KISIASA NA BADALA WAWE CHACHU YA MAENDELEO

          
 Wawakilishi wa vijana kutoka Afrika mashariki pamoja na balozi wa vijana          katika jumuiya ya Madola

Vijana katika nchi za Jumuiya ya Afrika mashariki wameanza kuonyesha hofu yao,juu ya namna wanavyotumiwa na baadhi ya wanasiasa, wenye maslahi binafsi katika kuleta machafuko, huku wakibainisha kutokuridhishwa na mwenendo wa ushirikishwaji, katika masuala ya maendeleo na uchumi.

Wawakilishi wa vijana kutoka Afrika mashariki pamoja na balozi wa vijana katika jumuiya ya Madola kwa pamoja wamekutaka katika Kituo cha Maendeleo ya Kimataifa cha MS TCDC-USA RIVER Arusha katika ushirikishwaji mpana zaidi unaolenga kuwafanya vijana waweze kuwa sehemu ya kupanga na kufanya maamuzi katika kuitengeneza Jumuiya.
Akizungumza katika majadiliano hayo,Mkuu wa Wilaya ya Arusha Nyirembe Munasa ameonya dhana ya kuwachukulia Vijana kama bomu linalosubiri kupasuaka na badala yake wafikiriwe kama rasilimali inayoweza kuijenga Afrika.
Kwa upande wake Mwakilishi wa Vijana kutoka nchini Kenya Noli Kaaya amesema kuwa vijana wanaweza kuwa wawakilishi wazuri wa taifa katika shughuli mbalimbali za kimaendeleo na uongozi katika kukuza uchumi.

0 comments:

Post a Comment

.

.

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...