WAY

Saturday, November 1, 2014

Serikali imetenga zaidi ya shilingi Bilion moja kwa ajili ya kununua vifaa vya Maabara zote zinazojengwa nchini

                             Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi Dk. Shukuru Kawambwa
Serikali imetenga zaidi ya shilingi Bilion moja kwa ajili ya kununua vifaa vya Maabara zote zinazojengwa nchini kwa lengo la kuboresha kiwango cha elimu na hasa katika shule za sekondari za kata ambazo zilikuwa hazina maabara.

Akiongea na wanachi mjini Bukoba Naibu wa Waziri wa Elimu Tamisemi Kasim majaliwa ambae alikuwa mgeni rasimi katika harambee ya kuchangisha pesa zitakzo tumika katika ujenzi wa maabara amesema zoezi la ujenzi wa maabara katika shule za sekondari si la wananchi pekee .

Mh. majaliwa ameongeza kuwa serikali imetenga bajeti ya zaidi ya sh. bilioni 1 ambazo zitatumika kununua vifaa vya maabara zote zinazojengwa nchini nakwamba zoezi la ujenzi wa maabara limekuwa likikabiliwa na changamoto mbalimbali ikiwemo uhaba wa fedha ambapo amewataka wadau wa elimu na taasisi mbalimbali zenye uzalendo na taifa wajitokeze ili kuchangia ujenzi huo.

Kwa Upande wake Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi Dk. Shukuru Kawambwa amesema Serikali imetangaza kutoa ajira za mkataba kwa walimu wastaafu wa masomo ya hisabati na sayansi ili kukabiliana na upungufu mkubwa wa walimu wa masomo hayo nchini huku akiwataka maafisa elimu wa mikoa nchini kuorodhesha walimu hao kwa ajili ya kuanza tarabu za kuwajiriwa

Wakati huo huo Serikali imetangaza rasmi kuanza mchakato wa kuwahamisha wanafunzi wa shule ya sekondari ya Oswald Mang’ombe Wilayani Butiama ili majengo ya shule hiyo yatumike kwa ajili ya chuo kikuu cha Mwalimu Julius Kambarage Nyerere wakati serikali ikikamilisha mchakato wa ujenzi wa chuo hicho cha sayansi na teknolijia katika kumuenzi

0 comments:

Post a Comment

.

.

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...