WAY

Tuesday, November 4, 2014

KURA YA MAONI KATIBA INAYOPENDEKEZWA NI APRIL 30, 2015- PRF. JK

                 
                                   Rais wa Tanzania Prof. Jakaya Kikwete
Rais wa Tanzania Prof. Jakaya Kikwete amewataka Watanzania kujitokeza kwa wingi Aprili 30 , 2015 kupiga kura ya maoni ya kapiga inayopendekezwa kwa kuzingatia maslahi mapana ya taifa na kwa vizazi vijavyo

Akiongea na wazee wa mkoa wa Dodoma hapo jana Prof Kikwete amesema Wananchi ndio wenye maamuzi ya mwisho kuhusu upatikanaji wa katiba mpya huku akiwataka wananchi kupata nakala za katiba inayopendekezwa ili waweze kuisoma na kuielewa ili kuwa na maamuzi sahihi wakati wa kupiga kura ya maoni.

Prof. Kikwete akizungumzia kuhusu uchaguzi wa serikali za mtaa amewataka wananchi kujitokeza kwa wingi katika kujiandikisha katika daftari la wapiga kura na kuwataka kutumia fursa hiyo kujitokeza katika kugombea katika nafasi mbalimbali za uongozi katika ngazi za serikali za mtaa.

0 comments:

Post a Comment

.

.

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...