WAY

Tuesday, November 4, 2014

TANZANIA YATUNGA KANUNI MPYA ZA UKAGUZI MAGARI KUPUNGUZA AJALI ZA BARABARANI

           
 Kamanda wa Polisi wa Kikosi cha Usalama Barabarani nchini Mohamed Mpinga

Jeshi la Polisi nchini Tanzania Kikosi cha Usalama Barabarani,kimewasilisha kanuni nne mpya za ukaguzi wa Magari nchini ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kukabiliana na Ongezeko la ajali za barabani hususani kwa magari yanayosafirisha abiria nchini.

Wakati akifungua majadiliano ya namna kanuini hivyo zitakavyosaidia kukabiliana na ajali hizo,Kamanda wa Polisi wa Kikosi cha Usalama Barabarani nchini Tanzania,Kamanda Mohamed Mpinga amesema kanuni hizo zitasaidia kuyabaini magari ambayo yamechakaa kwa kutumia mfumo wa kisasa.

Kwa upande wake aliyekuwa Mkurugenzi wa Mamlaka ya Usafiri wa nchi kavu na Majini SUMATRA,Ahmad Kilima amesema kanuni hizo zitaponguza ajali zisizo za lazima zinazosababishwa na uchakavu wa magari.

0 comments:

Post a Comment

.

.

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...