WAY

Monday, November 3, 2014

WAKAZI WAKIMBIA MAKAZI YAO KISA MICHANGO YA MAABARA YA SHULE ZA KATA

                      Mfano wa Maabara zinazotakiwa kuwepo nchini nzima
Baadhi ya Wananchi Wilayani Karagwe Mkoani Kagera nchini Tanzania wameyakimbia makazi yao kwa ajili ya Kukwepa kuchangishwa Michango kwa ajili ya Ujenzi wa Vyumba vya maabara katika shule za Kata.

Afisa Mtendaji wa Kata ya Nyakabanga Bw. John Bigimano na kusema kuwa Wanasiasa wanaohitaji kura ndio kimekua chanzo kikubwa cha wakazi hao kukimbia michango hiyo kwa kuwadanganya kuwa Serikali imetenga fedha nyingi kwa ajili ya ujenzi huo.

Bw. Bigemano ameongeza kuwa hali hiyo inafanya mapaka sasa katika Shule 19 ni shule 5 tu katika kata yake ndio zimeanza ujenzi wa maabara hizo ambapo kwa mujibu wa agizo la rais hadi mwishoni mwa mwezi huu shule zote ziwe zimekamilisha ujenzi huo.


0 comments:

Post a Comment

.

.

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...