WAY

Friday, October 31, 2014

SERIKALI YASEMA HAITAWAONDOA WANANCHI WA ARUMERU WENYE MGOGORO NA MWEKEZAJI

 
 Naibu wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mh. George Simbachawene
Serikali imesema haitawaondoa wanakijiji wa cha Singu kata ya Sigino katika Halmashauri ya Babati Mkoani Manyara nchini Tanzania ambao wana mgogoro na mwekezaji katika eneo hilo na kusema kuwa itawapanga katika utaratibu wa Mipango Miji.

Hayo yamezungumzwa na Naibu wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mh. George Simbachawene wakati alipotembelea wilayani humo katika kutafuta ufumbuzi na kutatua migogoro ya Ardhi wilayani humo.

Mh. Simbachawene amesema kuwa wakazi wa eneo hilo itabidi wakubali kutanuka kwa mji na kuweza kupewa hatua za kufanya katika kupanuka kwa halmshauri hiyo hivyo kuwataka waanze kujipanga katika kukabiliana na changamoto za kupanuka kwa Mji.


0 comments:

Post a Comment

.

.

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...