WAY

Thursday, October 16, 2014

MATAIRI CHAKAVU CHANZO CHA AJALI BARABARANI


                       GARI NA TAIRI CHAKAVU
Idadi kubwa ya wamiliki na madereva wa magari nchini Tanzania hawafahamu umri wa matumizi ya matairi ya magari, kiasi kwamba wengi wao huishia kununua matairi ambayo muda wake wa kutumika umekwisha na hivyo kusababisha ongezeko la ajali za barabarani.

Uchunguzi wa East Africa Radio umebaini kuwa kutokana na ukosefu wa uelewa, wanunuzi wa matairi mara nyingi wamekuwa wakiangalia zaidi upya na mwonekano wa matairi, badala ya alama za kitaalamu zinazoonyesha tarehe ya kutengenezwa pamoja na mwaka wa ukomo wa matumizi wa matairi husika.

East Africa Radio imefanya mahojiano na mfanyabiashara wa matairi Bw. Aloyce Aron, dereva wa muda mrefu mzee Kassimu Msisi na fundi wa magari Bw. Machimu Ludovick ambao walikuwa na haya ya kusema.

0 comments:

Post a Comment

.

.

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...