WAY

Friday, October 24, 2014

KUNA WAFANYAKAZI WALIFANIKISHA WIZI WA BENKI YA STANBIC-KOVA

                Kamanda kanda maalumu Dar es Salaam Kamishina Suleimani Kova
Watu wasiofahamika wanaosadikiwa kuwa ni Mjambazi jana walivamia Benki ya Stanbic katika tawi la Myfair jijini Dar es Salaam nchini Tanzania na kupora kiasi cha fedha ambacho kiasi chake bado hakijafahamika.

Akithibitisha kutokea kwa tukio hilo Kamanda wa wa jeshi la Polisi Kanda maalumu ya Dar es Salaam, Kamishana Suleiman Kova ameziagiza benki zote za jijini humo kuhakikisha zinalindwa na askari polisi ili kukabiliana na uhalifu unaojitokeza mara kwa mara.

Kamanda Kova pia amesema wizi huo unaonekana ni mpango uliofanywa na baadhi ya watumishi wa banki hiyo kutokana na wezi hao kufanya tukio hilo na kuchukua fedha kwa Urahisi Zaidi.

Aidha ameongeza kuwa waajiriwa wa mabenki hayo watafanyiwa uchunguzi pamoja na kuchukuliwa alama muhimu ikiwamo alama za vidole ili kukabiliana na uhalifu unaofanywa na baddhi ya watumishi wasiokuwa waaminifu.

Kova amesema kuwa katika uchugnuzi wa Awali wamegundua wizi wa mtandao wa ndani ya banki kwasababu hakuna nguvu iliyotumika na wakapata taarifa kutoka kuwa kuna watu wamefungiwa chooni lakini kuna vitufe vya kubonyeza vya hatari ili kutoa taarifa lakini havikubonyezwa.


0 comments:

Post a Comment

.

.

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...