WAY

Friday, October 24, 2014

MIFUKO YA JAMII YATAKIWA KUSAIDIA JAMII NA SIKUNYANG'ANYA WANACHAMA

                     Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Tamisemi Hawa Ghasia
Mifuko ya jamii hapa nchini imeshauriwa kuelekeza nguvu zaidi katika kuwahamasisha wananchi wasio katika sekta rasmi ili kuboresha maisha yao badala ya kuendelea kugombea wanachama walio katika sekta kama ilivyo hivi sasa.

Rai hiyo imetolewa na waziri wan chi ofisi ya waziri mkuu Tamisemi Hawa Ghasi wakati akifungua mkutano wa saba wa LAPF jijini Arusha unaowakutanisha wanachama wa mfuko huo waajiri na wadau wengine muhimu wa mfuko huo.

Aidha waziri Ghasia ameiomba LAPF kutazama upya uwezekano wa kuanza kutoa fao la elimu kwa wategemezi wa wanachama ili kuwapunguzia mzigo mkubwa wanchana wa kusomesha watoto ambao kwa sasa ni changamoto kubwa.

0 comments:

Post a Comment

.

.

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...