WAY

Monday, October 13, 2014

ASILIMIA 35 YA WATOTO NCHINI TANZANIA WAMESHAFANYIWA VITENDO VYA UKATILI



                                        Mkurugenzi LHRC, Dkt Hellen Kijo- Bisimba
Asilimia 35 ya watoto chini ya miaka 18 nchini Tanzania wamefanyiwa vitendo vya ukatili wa kijinsia ikiwa ni pamoja na kuolewa wakiwa na umri mdogo hali inayochangia kushindwa kumu kutunza familia.

Akizungumza jijini Dar es salaam,Mkurugenzi wa kituo cha Sheria na Haki za Bianadamu,Dkt. Hellen Kijo-Bisimba amesema mkoa wa shinyanga unaongoza kwa kuwa na idadi kubwa ya ndoa za utotoni kutokana na baadhi ya mila na desturi za wakazi wa mkoa huo.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Mtandao wa Kupinga ndoa za utotoni TCEMN, Justa Mwaituke amesema tatizo la ndoa za utotoni ni kubwa na linaathiri maendeleo kwa watoto wanaoolewa wakiwa na umri mdogo.


0 comments:

Post a Comment

.

.

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...