WAY

Friday, October 24, 2014

MFUMO WA ELIMU NDIO TATIZO LA AJIRA AFRIKA MASHARIKI

                         Mwenyekiti Baraza la Biashara Afrika Mashariki
Mwenyekiti wa baraza la biashara la nchi wanachama wa jumuiya ya afrika mashariki bw. Felexs Mosha amesema jitihada za kukabiliana na tatizo la ajira kwa vijana wakiwemo wanaomaliza Vyuo Vikuu zitakuwa na mafanikio kama serikali za nchi wanachama zitakubali kuwa na mfumo shirikishi wa elimu na unaozingatia mahitaji soko la ajira kwa sasa

Bw. Mosha ameyasema hayo katika mkutano wa baraza hilo la biashara na baraza la vyuo vikuu la afrika mashariki, ulioandaliwa kwa ushirkiano na benki ya Maendeleo ya Afrika Mashariki, unaofanyika Kigali, nchini Rwanda.

Katibu mtendaji wa Baraza hilo Prf. Mayunga Nkunya amesema pamoja na changamoto zinazowakaabili wahitimu wa vyuo vikuu katika nchi za Afrika Mashariki uchunguzi umeonyesha kuwa wana uwezo mkubwa wa kuleta mabadiliko kama mfumo uliopo utabadilika

0 comments:

Post a Comment

.

.

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...