WAY

Thursday, October 16, 2014


                      PROF. JUMMANNE MAGHEMBE
Idadi kubwa ya wakazi wa Tanzania hasa waishio maeneo ya vijijini wapo hatarini kuendelea kukosa maji safi na salama kutokana na kushindwa kutunza vyanzo vya maji hali inayochangiwa na shughuli za binadamu.

Hayo yameelezwa jana jijini Dar es Salaam na Waziri wa Maji Profesa Jumanne Maghembe wakati wa mkutano wa pamoja wa wadau wa sekta ya maji, wenye lengo la kuangalia mafanikio yaliyopatikana katika awamu ya kwanza ya utekelezaji wa mpango wa miaka sita katika sekta hiyo.

Profesa Magembe amesema ni lazima serikali na wananchi kwa ujumla kutambua hali hiyo na kuchukua hatua za makusudi kutunza rasilimali hiyo kwa lengo la kuwa endelevu na amewataka wananchi kufuata sheria zinazoelekeza namna ya kuhifadhi vyanzo vya maji.

0 comments:

Post a Comment

.

.

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...