WAY

Thursday, February 26, 2015

ASKARI WATANO WAJERUHIWA VURUGU ZA IRINGA KATI YA ASKARI NA WANANCHI



     Kamanda wa Polisi Mkoa wa Iringa Ramadhani Mungi
Askari watano wamejeruhiwa kufuatia vurugu zilizotokea  baina ya jeshi la polisi pamoja na wananchi katika mji wa Ilula kijiji cha dinginayo wilaya ya kilolo mkoani iringa pamoja na raia wawili kujeruhiwa.

Kaimu kamanda wa jeshi la polisi PUDENSIANA PROTAS amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kusema kuwa tayari jeshi la polis linawashikilia watuhumiwa kumi na nane kwa mahojiano huku upelelezi ukiendelea.

Tukio hilo limetokea majira ya saa 4 asubuhi na limesababisha kifo cha mwanamke mmoja aliyefahamika kwa jina la mwanne mtandi na katika vurugu hizo kumesababisha uharibifu wa mali za jeshi la polisi ambayo ni gari,pikipiki pamoja na gari moja ambayo ilikuwa ni kielelezo katika kituo pamoja na kuharibu jingo la polis kwa kuvunja vioo.

Aidha kamanda amesema kuwa fujo hizo zilisababishwa na oparationi kuhusu uuzaji wa pombe za kienyeji na makosa mbalimbali kwa wananchi huku akiwataka wananchi kutokujichukulia sheria mkononi ili kuepusha majanga kama hayo.

0 comments:

Post a Comment

.

.

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...