WAY

Thursday, February 26, 2015

MAHAKAMA KUU YAKALIA SHAURI LINALOTAKA SERIKALI KUTOA ULINZI KWA JAMII YA ALBINO.

 Mkurugenzi wa kituo cha haki za Binadamu Helen-Kijo Bisimba
Mahakama Kuu ya Tanzania imeshindwa kusikiliza kesi ya kikatiba iliyofunguliwa na Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu kwa kipindi cha miaka saba iliyopita,

shauri ambalo kituo hicho kinaitaka mahakama iilazimishe serikali kutoa ulinzi wa uhakika kwa watu wenye ulemavu wa ngozi nchini maarufu kama albino.

Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo hicho Dkt. Hellen Kijo-Bisimba, amesema hayo leo katika mahojiano na East Africa Radio na kufafanua kuwa kuchelewa kusikilizwa kwa kesi hiyo kwa namna moja inaweza kuwa imechangia kuzorota kwa usalama dhidi ya jamii ya albino nchini.

Kwa mujibu wa Dkt. Bisimba, matukio ya ukatili dhidi ya albino nchini yanayoendelea hivi sasa yanahitaji mbinu na njia nyingi katika kukabiliana nayo, mojawapo ikiwa ni ulinzi wa uhakika kwa jamii hiyo ya Watanzania.

0 comments:

Post a Comment

.

.

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...