WAY

Tuesday, February 10, 2015

TANZANIA YASHUTUMIWA KUWAFADHILI WAASI WA FDLR KUPANGA MASHAMBULIZI CONGO

                      Rais wa Jamhuri ya Muungano wa TanzaniaJakaya Kikwete
 Umoja wa mataifa imezituhumu serikali za Tanzania na Burundi kuhusiana na hali katika Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo.

Ripoti mpya ya kundi la wataalamu wa umoja huo kuhusu Congo, imeituhumu Tanzania kwa kuwaruhusu viongozi wa kundi la waasi wa FDLR kuandaa mikutano nchini humo.

Taarifa hiyo ya Umoja wa mataifa inasema kuwa tangu mwaka wa 2013, viongozi wa FDLR na baadhi ya washirika wao wa kisiasa kutoka Ulaya wamekuwa wakikutana nchini Tanzania.

Hata Hivyo katika kujibu madai hayo serikali ya Tanzania ilikanusha kabisa kuwahi kuakaribisha mikutano yoyote ya waasi ndani ya ardhi yake na kuongeza kuwa hakujawahi kuwa na mazungumzo yoyote kati ya majeshi yake na wapiganaji wa FDLR.

0 comments:

Post a Comment

.

.

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...