WAY

Tuesday, February 24, 2015

HAJI RAMADHANI AIBUKA NA BABY LOVE ASEMA ANAAMINI ITALETA MAPINDUZI KATIKA TASNIA YA MUZIKI ATAMBA KUACHIA NYIMBO BAADA YA NYIMBO

                
                  Haji Ramadhani Makuke akiwajibika Jukwaani
Msaanii wa Kizazi kipya alitokea kwenye mashindano ya kuibua vipaji Bss na sasa anatamba na band ya Twanga Pepeta Haji Ramadhani Makuke amekuja na ujio mpya wa kazi nje ya band yake na kuachia Singo mpya alioipa jina mpya la BABY LOVE.

Haji amesema nyimbo hiyo ina vionjo vya kiasili amesema ameitoa ili kuwaonyesha watanzania kipaji kingine tofauti katika uimbaji na pia kuleta ladha mpya katika muziki wa kizazi Kipya.

Hajji amesema ameamua kufanya kazi kwenye band na nje ya band kama Solo ili kujiongezea mashabiki na pia kubadilisha ladha ya mziki ila pia kujitafutia kipato kutokana kuuza nyimbo kwa mtindo wa singo kwa kuwa album kwa sasa ni ngumu kuuzika.

0 comments:

Post a Comment

.

.

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...