WAY

Wednesday, February 25, 2015

WANAWAKE WANASHINDWA KUTAMBA KATIKA MUZIKI KUTOKANA NA UKIRITIMBA ULIOPO KATIKA TASNIA


         Deborah Nyangi akiitumikia Kalunde Band.
Mwanadada anaetamba na Band ya Kalunde Band, Deborah Nyangi ambae anatikisa na wimbo wake wa FINGO amesema wanawake wanashindwa kutamba katika game la muziki wa kizazi kipya kutoka na ukiritimba uliopo katika tasnia.

Nyangi amesema anaamini kuna vipaji vingi sana vya kuimba kwa watoto wa kike ila tayari wameshajenga woga wa kujitokeza kutokana na kuamini kwamba ukitaka kufanya vizuri lazima uhonge kama sio pesa basi hata kutumia mwili wake.

Nyangi ambae kwa sasa anajipanga kuachia wimbo wake mpya amewataka watoto wa kike wajiamini kwa kile wanachokifanya na wasikubali kuyumbishwa na watu wachache ambao wanajihisi wameshikilia game ila kazi nzuri ndio itawafikisha wanapotaka.

0 comments:

Post a Comment

.

.

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...