WAY

Monday, February 23, 2015

WAANDISHI WA HABARI WATAKIWA KUTUMIA KALAMU ZAO KUFICHUA MAUAJI YA ALBINO

                          Waandishi wa habari wakiwa kazini kwenye mkutano

 Waandishi wa habari nchini, wametakiwa kutumia kalamu zao kufichua chanzo cha mauaji ya watu wenye ulemavu wa ngozi Albino, ambao umeibuka kwa kasi kubwa siku za karibuni.

Akizungumza leo Mjini Moshi na waandishi wa habari kwenye warsha ya siku tatu iliyoandaliwa na Chama cha waandishi wa habari wanawake Tanzania, (TAMWA),kwa lengo la kufichua ukatili wa kijinsia, Mshauri wa vyombo vya habari, Deo Peter, alisema kuna hajana ya kufichua chanzo cha mauaji hayo.

Amesema inasikitisha kuona watu hao wanaendelea kuuwawa kikatili, huku waandishi wakijikita kuandika tu jinsi wanavyouwawa, bila kufanya utafiti kujua chanzo cha mauaji hayo ni nini, jamo ambalo halisaidii kukomesha kiini cha mauaji hayo.
 
Aidha amesema sambamba na hilo pia hata kwenye seuala la ukeketaji nao waandishi wa habari wakijikita kufichua chanzo cha ukeketaji katika jamii husika ni zipi itasaidia kukomesha pia ukeketaji.

Amesema ukatili wowote ule unapofanyika unamyima mtu kukosa uhuru na kinaleta athari za kisaikolojia miongoni mwa wahusika wa ukatili huo.

Naye Mwakilishi wa Chama cha Waandishi wa Habari Wanawake Tanzania (TAMWA),ambaye alikuwepo katika warsha hiyo kwa niaba ya Mkurugenzi wa Tamwa, Judica Losai, amesema kuwa wanahabari wanapaswa kuunganisha nguvu ili kufichua ukatili wa kijinsia ambao kwa sasa umeshika kasi
kubwa.

Amesema kinachopaswa kuzingatiwa katika uandishi wa habari za kufichu  ukatili wa kijinsia ni umakini, kuzingatia lugha ya kutumia na kuhakikisha waathirika wanapata msaada mwisho wa siku.

Amesema kuwa ukatili wa kijinsia nchini mkubwa ambao kwa mujibu wa takwimu za Wizara ya Afya za mwaka 2013 inaonyesha Mkoa wa Manyara unaongoza ukeketaji kwa asilimia 71, ikifuatiwa na Dodoma asimilia 64 na Arusha asilimia 59.

0 comments:

Post a Comment

.

.

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...