WAY

Monday, December 15, 2014

AUAWA KWA KUPIGWA RISASI NA POLISI WAKATI WA VURUGU ZA UCHAGUZI MKOANI TABORA


  Kamanda wa polosi mkoa wa Tabora kamishna msaidizi wa polisi Suzan Kaganda

Mtu mmoja aliefahamika kwa jina Batholomeo Edward mkazi wa mtaa wa majengo mjini Nzega mkoani Tabora amefariki dunia na mwingine kujeruhiwa vibaya kwa kupigwa risasi na askari wa jeshi la polisi wakati wakisubiri matokeo ya uchaguzi baada ya kupiga kura katika uchaguzi wa serikali za mitaa uliofanyika jana kote nchini.

Kaimu Mganga Mfawidhi wa hospitali ya serikali ya wilaya ya Nzega Dkt. Joseph Bahati amesema hospitali yake imepokea majeruhi wawili majira ya saa 11.00 alfajiri mmoja akiwa amejeruhiwa tumboni na kitu chenye ncha kali kilichotowa utumbo wake na mwingine ubavu na mkono wa kushoto na kuwa wakiwa wanapewa matibabu mmoja wao akafariki dunia kutokana na kutokwa damu nyingi.

Kwa mujibu wa mashuhuda wa tukio hilo limetokea majira ya saa 10.00 alfajiri katika mtaa wa majengo ambapo baadhi ya wakazi wa eneo hilo wakiwa wakisubiri matokeo msimamizi wa uchaguzi alimtangaza mgombea wa CCM, kuwa mshindi hali iliyosababisha taharuki miongoni mwa vijana na hivyo askari wa jeshi la polisi kuingilia kati na kuanza kuwatawanya kwa kupiga mabomu ya machozi hewani na baadae kupiga risasi za moto na kuwajeruhi Batholomeo Edward na Lucas Daudi ambao wanadaiwa kuwa ni wafuasi wa umoja wa katiba ya wananchi (ukawa).

Viongozi wa Umoja wa Katiba ya Wananchi (UKAWA) Wilayani Nzega wamelaani vikali kitendo cha jeshi la polisi kutumia silaha za moto kuwatawanya watu waliokuwa wakishangilia ushindi na hatimaye kusababisha mauaji hayo na kuwa suala hilo watalifikisha kwenye vyombo vya sheria ili iweze kuchukua mkondo wake.

Akizungumza kwa njia ya simu Kamanda wa Polisi mkoa wa Tabora Bi. Suzan Kaganda amethibitisha askari wa jeshi lake kutumia mabomu ya machozi na risasi za moto zilizopigwa juu kutawanya mkusanyiko wa watu waliokuwepo eneo hilo.

0 comments:

Post a Comment

.

.

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...