WAY

Tuesday, December 16, 2014

DKT. SHEIN AWATAKA WAFANYABIASHARA ZANZIBAR KUWA WABUNIFU

                   Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt. Ali Mohamed Shein
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt. Ali Mohamed Shein amewataka wafanyabiashara wa Zanzibar kuwa wabunifu na wajasiriamali wa kuibua maeneo mapya ya biashara na kuondoakna na mfumo wa kulingana.

Dkt. Shein ametoa changamoto hiyo wakati akizindua mkutano wa nane wa baraza la biashara la Zanzibar ambapo amesema Wafanyabishara wengi wamekuwa biashara zao zinalingana hali inayosababisha kuwepo mazingira magumu na amewataka wabuni maeneo mapya

Mapema waziri wa Biashara ,Viwanda na Masoko Mhe Nassor Ahmed Mazrui alieleza mafanikio na mikakati ya baraza hilo la biashara ambapo amesema ushirikiano wa sekta binafsi na seriklai umeongezeka.

Baadhi ya wafanyabishara nao walipata fursa ya kuelezea hali halisi ya mfumo wa biashara unavyokwenda nchini.

huu ni mkutano wa nane wa baraza la biashara la Zanzibar ambapo mwenyekiti wake na huwa rais wa Zanzibar na kauli mbiu ya mwaka huu ni uimarishaji wa mazingira ya biashara zanzibar na unahudhuriwa na viongozi na wafanyabisharawa zanzibar.

0 comments:

Post a Comment

.

.

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...