WAY

Monday, December 15, 2014

MJUMBE CHADEMA AKUTWA AMEKUFA BAADA YA KUTANGAZWA MSHINDI


Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) mkoani Geita, kimepata pigo baada ya mshindi wa nafasi ya ujumbe wa viti maalum katika uchaguzi uliofanyika jana Jumapili katika mtaa wa Msalala Geita mjini, Bertha Chimani miaka 32, kukutwa katika shimo la choo lisilotumika akiwa amefariki dunia.

Chimani ambaye alipata kura nyingi katika uchaguzi huo, aliwaaga wenzake waliokuwa wakisubiri kushangilia ushindi huo akiwamo dada yake kuwa anakwenda kujisaidia lakini hakuweza hakurejea mpaka mwili wake ulipogundulika jana asubuhi.
Mwili wake ulikutwa ukielea katika shimo la choo kilichokuwa hakijafunikwa ndani ya uzio wa jengo lililokuwa linatumika kwa ajili ya kupigia na kuhesabia kura lenye urefu wa zaidi ya futi 30.

Kamanda wa polisi mkoa wa Geita, Joseph Konyo, amethibitisha kutokea tukio hilo na kudai marehemu alitumbukia katika shimo hilo usiku na mwili wake uliopolewa na kikosi cha zimamoto na kuhifadhiwa chumba cha kuhifadhia maiti cha hospitali ya wilaya ya Geita kwa uchunguzi zaidi.

Katika tukio lingine lililotokea leo, Simeo Isaka miaka 42, mkazi wa kijiji cha Ngokolo kata ya Bukomela tarafa ya Mweli wilayani Kahama, ameuawa kwa kukatwa na jembe kichwani wakati akishangilia matokeo ya ushindi wa chama chake cha Chadema.

Kamanda wa Polisi mkoani Shinyanga, Justus Kamugisha, amesema tukio hilo limetokea usiku wa kuamkia leo wakati Isaka akishangilia matokeo ya uchaguzi wa serikali za mitaa wa kijiji cha Ngokolo.

0 comments:

Post a Comment

.

.

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...