WAY

Tuesday, December 30, 2014

MWAKYEMBE AMTAKA MKURUGENZI TICTS KUJIELEZA JUU YA GHARAMA ZA UTOAJI WA MIZIGO

Waziri wa Uchukuzi Dkt, Harrison Mwakyembe

Serikali ya Tanzania imesema udhibiti wa vitendo vya wizi pamoja na idadi ya wateja wanaotumia bandari kumechangia kuongezeka kwa kiwango cha mapato kutoka shilingi bilioni 428 mwaka 2012 hadi kufikia shilingi bilioni 529 Juni mwaka huu.

Akizungumza jana jijini Dar es salaam Waziri wa Uchukuzi Dr. Harrison Mwakyembe katika mkutano wake na wadau wa sekta ya uchukuzi wakiwemo wawakilishi wa wafanyabiashara kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo na kuongeza kuwa pia Mizigo nayo ikiongezeka toka Tani Million 13.7 mwaka jana na kufikia Tani Million 15.4 mwaka huu iliyoingia kupitia bandari hiyo

Kwa upande Mwingine Mwakyembe amemtaka Mkurugenzi wa Kampuni ya Kimataifa ya Huduma za Makontena katika bandari ya Dar es Salaam – TICTS, kufika kesho saa mbili kamili asubuhi,ofisini kwa waziri kutoa maelezo kuhusiana na tuhuma kuwa kampuni yake imekuwa ikitoza gharama za juu kubadilishia fedha za kigeni tofauti na viwango vinavyotolewa na benki kuu ya Tanzania.

Kwa upande wao Wafanyaiashara toka Jamhuri ya kidemokrasia ya Congo wameulalamika mfumo mpya wa utoaji na uingizaji migizo bandarini unaosimamiwa na mamlaka ya mapato Tanzania kuwa umekuwa ukisababisha usumbufu na gharama zisizo na msingi, tuhuma ambazo zimeungwa mkono na wamiliki wa bandari za nchi kavu nchini.

0 comments:

Post a Comment

.

.

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...