WAY

Tuesday, December 23, 2014

CHADEMA CHAKOSOA MAAMUZI YA RAIS JAKAYA KIKWETE

                             Katibu Mkuu wa Chadema Dkt. Wilbrod Slaa
Chama cha siasa upinzani cha Chadema, kimekosoa maamuzi ya rais Jakaya Mrisho Kikwete kuhusu kashfa ya ubadhirifu wa fedha katika akaunti ya Tegeta Escrow kwa madai kuwa hatua alizochukua hazikuzingatia maazimio ya bunge.

Akizungumza na vyombo vya habari jijini Dar es Salaam leo, Katibu Mkuu wa Chadema Dkt. Wilbrod Slaa amesema rais Kikwete ameshindwa pia kutumia mamlaka ya kinidhamu aliyopewa na Katiba, kwa kushindwa kuwawajibisha watuhumiwa wa kashfa hiyo hasa majaji wanaotuhumiwa kuhusika katika sakata hilo.

Kwa mujibu wa Dkt. Slaa, hata utenguzi wa nafasi ya Waziri wa Ardhi, Profesa Anna Tibaijuka haukufanyika kwa kuzingatia misingi ya utawala na kwamba hata kitendo cha kumweka kiporo Waziri wa Nishati na Madini Profesa Sospeter Muhongo nacho kinaonyesha jinsi serikali ilivyoshindwa kutekeleza maazimio ya bunge kuhusu hatua zinazostahili kuchukuliwa watuhumiwa wa Escrow.

Hivi karibuni Bunge la Tanzania liliapitisha maazimio nane ambapo miongoni mwa maazimio hayo ilikuwa ni pamoja na serikali kuwachukulia hatua ZA kinidhamu pamoja na kuwafuta kazi mawaziri na maafisa wa serikali waliohusika katika sakata hilo.

0 comments:

Post a Comment

.

.

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...