WAY

Tuesday, January 21, 2014

Wazazi wilayani MASASI wametakiwa kuipa eilimu kipaumbele

MASASI 20/1/2014
Wazazi wilayani MASASI wametakiwa kuipa eilimu kipaumbele,sambamba na kuacha mitazamo hasi na potofu.
Hayo yameelezwa na mwalimu mkuu wa  shule ya msing CHIGUGU wilayani Masasi Bw.YOHANA ABUNUAS wakati akizungumza na safari radio ofisini kwake.

ABUNUAS amesema miongoni mwa changamoto kubwa wanazo kumbanana nazo wilayani Masasi ni mwamko mdogo wa wazazi wa kutambua umuhimu wa elimu kwa watoto wao,kama wazazi wataipa elimu kipaumbele elimu itakua mkombozi kwa vijana wengi hapa nchini.

Aidha amelaani kitendo cha baadhi ya wazazi na walezi kupuuza umuhimu wa elimu na kushindwa kupeleka watoto wao shule pasipo sababu yeyote ya msingi.

Katika Hali isiyo ya kawaida shule ya msingi CHIGUGU hadi kufikia January 17 mwaka huu jumla ya watoto 35 pekee ndio wameandikishwa darasa la kwanza ,huku matarajio ya shule hiyo ikiwa ni kuandikisha watoto 135 wasajiliwe darasa la kwanza.

Kufuatia hali hiyo ABUNUAS amewahimiza wazazi na walezi wenye watoto wanao stahili kuingia darasa la kwanza wapelekwe  shule kwani hiyo ni haki yao ya msingi.
BEATRICE RIWA



0 comments:

Post a Comment

.

.

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...